Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Amir wa Kuwait ametoa amri rasmi ya kufuta uraia wa Ayatullah Sheikh Hussein Al-Matouq, mwanazuoni mashuhuri wa Kishia, pamoja na wanaharakati wengine watano wa kisiasa na kiraia.
Hatua hiyo imechukuliwa katika mfululizo wa hatua za kisheria zinazohusishwa na kesi za kiusalama dhidi ya baadhi ya watu wanaoikosoa serikali, kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa kuhusu uamuzi huo.
Baada ya uamuzi huo, baadhi ya wanaharakati walioathirika, akiwemo Mohammed Al-Mutair na Lulwa Al-Hussein, wamekosoa vikali hatua hiyo, wakiitaja kuwa ni uvamizi dhidi ya haki zao na ishara ya kile walichokiita utawala wa kipindi kibaya zaidi cha kisiasa katika historia ya Kuwait.
Maoni yako